Rais Kikwete akiwa na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe Bill Clinto ambaye yuko nchini kwa ziara ya kukagua miradi inayoendeshwa na taasisi yake ya Clinton Foundation katika nchi kadhaa za Afrika

Katika msafara wa Mhe Bill Clinton kuna mastaa kadhaa wa sinema basketball ambao wameongozana na Rais huyo mstaafu wa Marekani aliye katika ziara ya kikazi kukagua na kuendeleza kazi za maendeleo zinazofanywa barani Afrika na taaisis yake ya Clinton Foundation. Pichani juu kulia ni mcheza sinema nyota Dakota Fanning akiongea na mcheza sinema mwingine nyota Jesse Eisenberg na nyuma yao aliyekwenda juu ni mcheza basketball katika NBA Brook Lopez
 Jesse Eisenberg na Dakota Fanning wakishuhudia utiwaji saini wa mkataba wa maelewano kati ya Serikali ya Tanzania na tasisi ya Clinton Foundation Ikulu jijini Dar es salaam 
 Ankal akiwa na Jesse Eisenberg
Ankal akila pozi na Brook Lopez ambaye kenda hewani 
kama Hasheem Thabeet

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Hawa wamarekani wanazidi kumuongezea hasiri mheshimiwa sana rais Kagame.

    ReplyDelete
  2. Yano bado Jimmy carter na Bush baba ili kukamilisha idadi ya marais wote wa USA wanoishi.

    ReplyDelete
  3. What has this to do with Kagame? These are just planned visit and Clinton will visit Rwanda as well.

    ReplyDelete
  4. Nadhani mdau hapo juu Jimmy carter ameshafika Tanzania miaka ya sabini. Naomba wadau mnirekebishe katika hili kama nimekosea. Bado Bush baba tu.

    ReplyDelete
  5. Sasa Tanzania imejulikana Duniani, hata watalii watazidi sana mwaka huu, kwasababu Rais Kikweti ameitangaza nchi kwa ujio wa Rais Obama.

    ReplyDelete
  6. Huyo Jesse ndiye yule star wa movie ya Facebook aliyeigiza kama Zuckberg eenh??

    ReplyDelete
  7. kuingia ni rahisi kutoka sasa ngoja tutaona mwisho wake hatimaye litakuwa shamba la wamarekani nyanya ,kabeji mchicha utatoka hapa kwenda marekani kama ilivyokuwa zimbabwe shamba la uingereza.cha msingi watu wamilikishwe ardhi ili mwekezaji aungane na wazawa sio mwekezaji amilikishwe rasilimali

    ReplyDelete
  8. Bush tayari au unamsema Bush baba'ke? Duu yaani Mungu kaumba binadamu kutofautiana! Ankal huyo jamaa unamfikia tumboni !! Kweli si mchezo!! Teh teh teh!!

    ReplyDelete
  9. Hii si bure lazima tujipange kwa kichwa. Unajua tuwe smart ktk kushirikiana na Marekani wao wameshaamua hapo wanatoa msisitizo tu. Tukijinga vizuri kuhakikisha kuna win-win tutafika nao mbali,wenzetu S.Korea, Japan Na China wamefanikiwa kihivyo. Elimu ipewe kipao mbele ili kuandaa skilled labour, viongozi tuachana na bogus agreements ya akina Chenge, tuachane Na mentality ya misaada ambayo inakufanya uwe weak partner Bali tuangalie kwa makini kwa kila hatua nchi inafaikaje. Tuhusishe wazalendo ktk majadiliano ya mikataba, kunahaja ya kuunda timu maalumu ya kitaifa kupitia rasimu za mikataba ya kiuwekezaji kabla ya kusainiwa. Timu hiyo ijumuishe na wakereketwa kutoka hata kwenye vyama vya upinzani ili tusikosei mahali, jamani tunatakiwa kujenga nchi yetu kwa umakini ukubwa na tuwe na mtazamo wa miaka 500 ijayo. Hizo rasilimali zilizopo zitakapoisha na hatujafanya maendeleo yakueleweka basi taifa litadharauliwa mno duniani. Mungu ibariki Tanzania.

    ReplyDelete
  10. Ankal chini ya mti wa mbuyu..

    ReplyDelete
  11. Mdau wa No.1 na No.3 Raisi Kagame ametopoza umaarufu ktk Jumuiya ya Kimataifa kwa Kitendo chek cha siri cha kushiriki ule Ujambazi Mahsariki ya Kongo kwa kuwasaidia M-23.

    Licha ya Maendeleo anayosifiwa kuleta nchini kwake na mafanaikio lakini nyuma yake pana Kivuli kichafu.

    Hapo ndio pale unakuta Kiongozi Mkuu wa Dini anashiriki Ujambazi!

    ReplyDelete
  12. Ikiwa unachakuuza na Mmarekani basi atashirikiana na wewe. Ukiwa huna kitu atakwambia bye!!

    ReplyDelete
  13. Nilifikiri Ankal ame-shrink kwa ajili ya swaumu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...